Jinsi ya kuwasha GPS kwenye Smartphone
Ni rahisi kuwasha gps kwenye simu
Upande wa juu wa screen unaoonyesha tarehe, network ya simu nk
Iguse hiyo sehemu kwa kushusha chini
Utaona machaguo mengi kama kuwasha data, bluetooth, wi-fi, tochi na vitu vingine
GPS hutambulika kama Location
Ukigusa tu basi gps receiver ya simu itaanza kusoma eneo ulilopo
Na unaweza ukaona eneo ulilopo kwa kufungua ramani ya Google
Itakuonyesha ulipo kwa wakati huo
Usahihi wa GPS kuonyesha Eneo
Mfumo unatoa kwa usahihi mkubwa taarifa za eneo ambalo simu ipo
Ila si kwa usahihi wa asilimia mia
GPS huwa ipo nyuma kwa umbali wa mita tano toka eneo ambalo kifaa cha gps kilipo
Tatizo linakuwepo hasa pale simu inakuwa inapata data kutoka kwenye setilaiti chache
Tatizo hili linalekebeshwa kwa kuiwezesha simu janja kusapoti mifumo kama ya GPS ya nchi zingine
Ndio maana simu nyingi za daraja la kati na juu huwa zina mifumo zaidi ya mmoja ya utambuzi wa maeneo
Utakuta simu moja inakubali Galileo ya umoja wa ulaya, Glonass ya urusi na Beidou ya china
Kama utakuwa na matumizi mengi ya GPS inafaa ukawa na simu inayokubali mifumo mingi
Matumizi ya GPS na Faida Zake
Taarifa za GPS zinaweza kukusaidia kwenye mengi mno
Ukiwa umeiwasha itakusaidia kujua spidi ya chombo chochote cha usafiri unachosafiria ikiwemo baiskeli
Hilo linafanikiswa kwa kutumia aplikesheni
Kuna app nyingi zinazoweza kuonyesha spidi na umbali kutumia gps
Moja ya app iyo inaitwa GPS speedometer
Pia, inaimarisha ulinzi hasa pale simu inapopotea
Kama gps ikiwa imewashwa utaweza kufuatilia eneo ambalo simu ipo
GPS pia hutumika kupima viwanja
Je Ni Salama kuwasha GPS muda wote?
Kiujumla ni salama kama wewe si muharifu
Ubaya wa kuwasha gps mara kwa mara unakuja kwa makampuni makubwa ya teknolojia kama Google, Facebook, Apple nk
Yana tabia ya kuchota taarifa zako pasipo kujua japokuwa wengi hurusu hizo app kuchota data
Haya makampuni hutumia hizo taarifa kwenye biashara zao za matangazo
Mtu akiweka tangazo anaweza kuchagua eneo ambalo tangazo linapaswa lionekane
Kiujumla, ni vizruri GPS ikawa ON muda wote
Inakupa urahisi kuifutalia simu inapopotea.
Endelea kuwa nasi Share App ya TUTECH pia Jiunge nasi Telegram @Samalentvtech