Dondoo Fupi za Jinsi ya Kubeti na Kushinda mikeka yako
Kwanza, ngoja tupitie dondoo zinazojulikana zaidi ambazo zitakusaidia kupunguza idadi ya makosa unayoyafanya na kuzidi kujiongezea nafasi ya kushinda kila siku ukiona dondoo hizi zimekusaidia tafadhali njoo toa ushuhuda wako kwa SAMALEN TV ni bure kabisa hatutakutoza kiasi chochote ila usiache kutoa shukrani fuata dondoo zifuatazo kabla hujaweka mkeka wako;
- Chagua michezo unayotaka kuicheza – kuliko kupoteza nguvu zako na ubunifu kuhangaika kucheza michezo mingi ni bora uchague mchezo mmoja ambao unauelewa vizuri zaidi na ubaki nao huohuo. Hii itakusaidia kuelewa mambo mbalimbali yanayohusiana na mchezo husika ili uweze kuweka mikeka ya ushindi.
- Dhibiti hisia zako – kubeti kwa mihemko ndiyo njia ya kwanza ya kuanza kupoteza pesa zako, na hata kupoteza mtaji wako wote wa kubeti, hata uwe ni shabiki wa timu husika kwa miaka mingapi lazima utulize akili kwanza kabla ya kufanya maamuzi ya kuweka mkeka, vilevile usiruhusu furaha au uchungu wa kupoteza mkeka mmoja ikunyime hamasa ya kucheza na kushinda mkeka mwingine.
- Usisahau kupumzika – ubora wa mkeka wako ni muhimu zaidi ya wingi wa mkeka wako, hivyo kama umechoka sana baada ya kuchambua mkeka uliopita kwa muda mrefu au una uchungu wa kupoteza mkeka mwingine ni bora uchukue muda kupumzika na kujipanga upya.
- Jifunze kutokana na makosa yako yaliyopita – kama wewe ni mgeni kwenye michezo ya bahati nasibu, basi lazima tu utafanya makosa ambayo utakuja kuyajutia baadaye, hivyo basi hauna haja ya kujilaumu sana pindi unapokosea kwani ni nafasi yako ya kuweza kujifunza.
- Fanya utafiti wa kutosha – moja ya dondoo muhimu zaidi za kubeti ni kufanya upembuzi na uchambuzi yakinifu kwenye kusuka na kupangilia mikeka yako, kufanya utafiti kuhusu takwimu za timu na wachezaji husika vitakusaidia kupata uelewa mkubwa zaidi wa kufanya maamuzi kamilifu.
YouTube 👉 SAMALEN TV YOUTUBE
Download App 👉TUTECH ANDROID APP